EXCLUSIVE: SAMATTA ATOA KAULI NZITO KABLA YA KUIKABILI MALAWI
Mbwana Samatta, mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania na klabu ya TP Mazembe ya nchini Congo DR
Mshambuliaji wa kimataifa wa 
Tanzania anaecheza soka la kulipwa kwenye klabu ya TP Mazembe ya nchini 
Congo DR amesema hatoshangaa endapo mashabiki wa soka nchini watawalaumu
 wachezaji wa Stars kwa kushindwa kuifunga Malawi kwenye mchezo wa leo.
Samata amesema Stars inabidi 
ishinde mchezo wake wa leo dhidi ya Malawi kwasababu viwango vya timu 
zote mbili vinalingana kwa kiasi kikubwa. Licha ya kusema Stars ni 
lazima ishinde mbele ya Malawi, lakini amesisitiza kuwa inabidi ishinde 
kwa idadi kubwa ya magoli huku yeye akikataa kuahidi chochote kwenye 
mchezo huo.
“Siwezi kuahidi chochote 
kwasababu ahadi ni deni na usipolitimiza ni dhambi, ila nadhani kwamba 
tunaenda kupambana na siichukulii Malawi kama Nigeria, nafikiri Malawi 
ni timu ya kiwango chetu na nita-appreciate watanzania kama watatulaumu 
kwanini hatujaifunga Malawi”, amesema Samatta ambaye tayari ameshafunga 
magoli sita baada ya kucheza mechi nane kwenye ligi ya vilabu bingwa 
barani Afrika.
“Lazima tuifunge Malawi hakuna 
matokeo mengine ambayo tunayataka na ni lazima tumfunge kwa idadi kubwa 
ya magoli, yani lazima iwe hivyo”, amesisitiza Samatta ambaye anatarajia
 kucheza fainali ya ligi ya mabingwa Afrika siku chache zijazo akiwa na 
TP Mazembe.


No comments