Chuchu Akataliwa kwa Akina Ray
Yamemkuta! Staa wa sinema za Kibongo, Chuchu Hans anadaiwa kukataliwa na baadhi ya ndugu wa mwandani wake, Vincent Kigosi ‘Ray’ hivyo kuzidi kufifia kwa penzi lao.
Kwa mujibu wa mmoja wa mashosti wa Chuchu, kwa sasa mwanamama huyo yupo kwenye kipindi kigumu kwa sababu ndugu wa Ray (kaka na dada) hawamkubali kwa sababu wanazozijua wao ikiwemo kigezo cha dini.
Alipotafutwa Chuchu juu ya madai hayo alifunguka: “Naomba muachane na hayo mambo, yanazidi kunipa wakati mgumu, tayari nina matatizo na ndugu wa upande wa Ray.”
Chanzo: GPL
No comments